King'ora cha Mwehu ni tamthilia inayoangazia matatizo yakiuchumi, kisiasa na kijamii yanayotokana na utawala mbaya waviongozi wa nchi ya Sifuri. Viongozi hawa hawana chochote walalolote la kuwafaidi wananchi au nchi zao. Kinachowaongoza niulafi na kupapia kila kinachopatikana nchini na kudai wana hakiya kusherehekea utamu wa Keki ya Taifa.Wanafanya hivi hukuwananchi wakiendelea kuumia, kuteseka na kudhalilishwa naumaskini, njaa, ukosefu wa ajira miongoni mwa matatizo mengiyaliyokuwapo tangu enzi za kupigania uhuru. Lakini wananchihawana njia ya kujinasua. Kila anayesema ng'we, anapata chamtema kuni.Mwehu anapoliza king'ora chake, wengi wanampuuza na kudhanini mwehu tu, lakini hoja zake zinapelekea kuzinduka kwa umma.Bi Kurwa na Mlevi wanajiunga na Mwehu, na hatimaye chachu yamabadiliko inakolea. Kumbe jamii inaweza kubadilishwa namwehu! Je, mwamko huu utazua kitu gani? Hii ni tamthilia yakimapinduzi. Ni kurunzi ya jamii.
Lieferbar
ISBN | 9789966315472 |
---|---|
Sprache | swa |
Cover | Kartonierter Einband (Kt) |
Verlag | Lightning Source Inc |
Jahr | 20161012 |
Dieser Artikel hat noch keine Bewertungen.